19 avril 2024

Kisima hiki ni chenu, Kitunwe vizuri

“Tunzeni kisima hiki cha maji kwa sababu ni chenu, mradi huu umegharimu zaidi ya faranga 40,000,000 za Burundi. Kisima hiki kimejengwa kwa ajili yenu nyote kwa tofauti zenu, Waislamu, Waprotestanti, Wakatoliki wa makundi yote watafaidika nacho. »

Huu ni ujumbe kutoka kwa Mheshimiwa Pontien HATUNGIMANA, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mshikamano wa Kitaifa, Masuala ya Jamii, Haki za Binadamu na Jinsia Jumamosi hii Februari 25, 2023 kuko kzenye kijiji cha Bukeye wilaya ya Nyanza-lac mkoani Makamba wakati wa makabidhiano rasmi ya kisima cha maji kilichojengwa na Jumuiya ya Kiislamu ya Ahmadiyya nchini Burundi.

 

Alimtaka meneja wa mradi wa ujenzi wa kisima hiki kinachotumia miale ya jua kusukuma maji, pamoja na kuendeleza mradi huo hadi kwenye vijiji vingine na mikoa mingine, afikirie miradi mingine ya utoaji wa mikopo midogo midogo inayowezesha maisha ya wanyonge hao kupata kipato.

 

Kwa kuona maji ni uhai, Meneja wa Mradi huo wakati huo huo Mwakilishi wa Jumuiya ya Kiislamu ya Ahmadiyya nchini Burundi Sheikh Ghulam Murtaza, alisema wapo katika harakati za kuendeleza mradi huo hadi kwenye vijiji vingine ndani ya mfumo wa kutoa maji safi ya kunywa kwa wanyonge.

SIYAWEZI Oscar, Mshauri wa Kiufundi wa msimamizi wa Nyanza-lac, alishukuru kuwekwa kwa kisima hiki kwa ajili ya wakazi wa kijiji cha Bukeye kwa sababu walikuwa wakichukua safari ndefu kutafuta maji safi ya kunywa.

 

Ikumbukwe kuwa hii ni mara ya kwanza kwa Wizara ya Mshikamano wa Kitaifa, Masuala ya Jamii, Haki za Binadamu na Jinsia, kwa kushirikiana na washirika wake, kutoa misaada ya aina hii kwa watu wanaoishi katika mazingira magumu.

Elie HARINDAVYI

Le Coordonnateur de la Cellule de Communication et d'Information du Ministère des Droits de la Personne Humaines, des Affaires Sociales et du Genre

Voir tous les articles de Elie HARINDAVYI →