26 avril 2024

Tuna furaha kuwa na Mrundi, Rais wa Jukwaa la Wanawake la Kikanda

“Tunafuraha kubwa kumchagua Mrundi kuongoza Jukwaa hili kwa sababu anaongoza Jukwaa la Kanda linalojumuisha nchi 12 za ICGLR na tutamuunga mkono kupitia shughuli zitakazofanywa katika ngazi ya kitaifa”.

Ndugu Felix NGENDABANYIKWA, Katibu Mkuu Wizara ya Mshikamano wa Kitaifa, Masuala ya Jamii, Haki za Binadamu na Jinsia (Picha na Elie HARINDAVYI)

Hayo yamebainishwa na Ndugu Felix NGENDABANYIKWA, Katibu Mkuu Wizara ya Mshikamano wa Kitaifa, Masuala ya Jamii, Haki za Binadamu na Jinsia mwishoni mwa Mkutano wa Baraza Kuu la Jukwaa la Wanawake katika kanda hii uliofanyika mjini Bujumbura kuanzia tarehe 18 hadi 20 Mei, 2022.

Mheshimiwa Felix NGENDABANYIKWA amesema kuwa kulikua na ajenda muhimu kwa sababu ililazimika kukutana na nchi 12 wanachama wa ICGLR kupitia vikao hivyo ili wabadilishe miundo iliyokuwepo katika ngazi ya kamati ya Jukwaa la Wanawake wa Kanda Hii.

Dk. Sabine NTAKARUTIMANA, Rais wa Jukwaa la Wanawake la Kikanda. kushoto (Picha na Chanel HARINGANJI)

Wakati wa chaguzi hizi, aliripoti kuwa mkuu wa Jukwaa hili, alichaguliwa kuwa Mrundi, Dk. Sabine NTAKARUTIMANA, Rais wa Jukwaa la Wanawake la Kikanda.

Alieleza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Burundi itamuunga mkono ili kuimarisha shughuli kupitia shughuli zitakazofanywa katika ngazi ya kitaifa.

Ikumbukwe kuwa Urais wa Jukwaa hili la Kikanda ulikuwa ukihakikishwa na Bibi Athia Moustafa kutoka Sudan.

Elie HARINDAVYI

Le Coordonnateur de la Cellule de Communication et d'Information du Ministère des Droits de la Personne Humaines, des Affaires Sociales et du Genre

Voir tous les articles de Elie HARINDAVYI →