1 juillet 2025

KAULI YA MHESHIMIWA WAZIRI WA HAKI ZA BINADAMU USTAWI WA JAMII NA JINSIA KUHUSU MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA MSICHANA, toleo la 2019

1. Mnamo Oktoba 11 ya kila mwaka, Burundi inajiunga na nchi zingine za ulimwenguni kusherehekea Siku ya Kimataifa ya Msichana. Ni siku ya kujiuliza, ya utetezi ya mwamko na ya kujitolea kwa msichana.

Mhashimiwa Waziri wa Haki za Binadamu, Ustawi wa Jamii na Jinsia Bwana Martin NIVYABANDI akisoma tanganzo kuhusu maadhimisho ya Sikuu Kuu ya Kimataifa ya Msichana (picha na Elie HARINDAVYI)

2. Leo, msichana wa Burundi anakabiliwa na changamoto kubwa: kutomaliza masomo darasani kama inavyotakiwa, na hivyo kutofika kwa ukuaji wake halisi.

3. Siku hii inakuja wakati ambapo Serikali ya Burundi inafurahiya uwepo wa mfumo wa udhibiti na njia zinazofaa kukuza na ulinzi wa wasichana. Tunanukuu kuanzishwa kwa shule ya msingi hadi mwaka tisa  ambayo inaruhusu wanafunzi kufikia ukomavu fulani kuelewa faida za kusoma. Kwa upande mwingine, kupata ujuzi muhimu unaowawezesha kujumuishwa kikamilifu katika maisha ya kiuchumi na kijamii bila ugumu.

4. Kwa hivyo mada ya maadhimisho yaliyochaguliwa kwa mwaka huu ni: « Kuhimiza maendeleo endelevu ya msichana wa Burundi ».

5. Mada hii inawataka watendaji wote wanaofanya kazi katika uwanja wa kukuza na kulinda wasichana kuwekeza zaidi katika kukuza haki zao, kinga yao na uundaji wa mazingira mazuri kwa maendeleo yake.

6. Kwa hivyo, wakati msichana anachukuliwa sawa sawa kama kaka yake katika familia, anapata elimu bora na haki zake zinalindwa, inamruhusu kutambua ndoto zake za maisha na kuweza kushiriki vizuri katika maendeleo ya nchi na familia yake kama mama anayestahili atakapofunga ndoa.

7. Ni katika muktadha huu kwamba Serikali ya Burundi inafanya kazi ya kulinda haki za wasichana na kuinua ufahamu wao ili wawe na heshima waachane na tabia ya upotevu, ila waweze kushiriki katika shughuli za maendeleo binafsi.

8. Nchini Burundi, sherehe rasmi za kuadhimisha siku kuu hiyo  zitafanyika tarehe 11 Oktoba, 2019 huko Gitega, mji mkuu wa kisiasa wa nchi yetu, katika maeneo ya  shule ya ufundi wa manesi ya Gitega.

9. Tunatoa wito kwa warundi wote kuja kwa wingi kwenye sherehe hizo hasa wakaaji wa Gitega na kuunga mkono kila msichana, aweze kupambana na Umasikini ili afike mahali pamaendeleo yake.

10. Tunawatakieni siku kuu Njema yenye furaha kwa wasichana wote

11. Asante! Mungu awakubariki!

 

Elie HARINDAVYI

Le Coordonnateur de la Cellule de Communication et d'Information du Ministère des Droits de la Personne Humaines, des Affaires Sociales et du Genre

Voir tous les articles de Elie HARINDAVYI →